Monday, September 2, 2013

Mourinho apuuza ushindi wa Bayern



 31 Agosti, 2013 

Bayern Munich dhidi ya Chelsea
Bayern Munich dhidi ya Chelsea
Jose Mourinho alidai baada ya mechi kua timu bora ndiyo iliyopoteza kufuatia ushindi wa Bayern Munich dhidi ya watu 10 wa Chelsea kwa matuta 5-4 kufuatia suluhu ya bao 2-2 katika mchuano wa kombe la Uefa la Super Cup.
Chelsea ilionekana kukaribia ushindi zikiwa zimesalia sekunde chache kipenga cha kumaliza mechi kipigwe mjini Prague, lakini mchezaji aliyeingizwa katika mda wa majeruhi Javi Martinez akarudisha na kusababisha mda wa ziada na hivyo kusababisha mshindi aamuliwe kwa njia ya matuta.
Mchezaji Romelu Lukaku ndiye aliyekosa mkwaju wa mwisho ambao ungeamua mshindi lakini Mourinho hata hivyo kama kawaida alionekana kua katika hali ya ubabe bila kutaka kukubali matokeo.
"timu bora wazi wazi imepoteza," alisema. "wametushinda kwa sababu ya kufunga mkwaju mmoja zaidi yetu."
Awali mshambuliaji Fernando Torres aliipa Chelsea bao la kwanza katika kipindi cha kwanza lakini Franck Ribery akarudisha dakika mbili baada ya kipindi cha pili kuanza na kupelekea mchezo uingia mda wa ziada.
Mnamo dakika ya 85 mcheza kiungo Ramires akaonyeshwa kadi nyekundu na kuwaacha washindi wa Ligi ya Europa League uchi. Ingawa Eden Hazard aliirejeshea Chelsea matumaini katika kipindi hiki cha ziada, Martinez aliusukuma mpira wavuni sekunde chache kabla ya kipenga cha mwisho kusababisha mechi kuamuliwa kupitia matuta.

Man United wafungwa na watani wa jadi kuwndeleza mwanzo wa kusua sua wa man united na Livepool



 1 Septemba, 2013 
Liverpool waichapa Manchester United
Liverpool imejiweka katika nafasi nzuri sana kwenye ligi ya Uingereza baada ya kuwazima mabingwa wa ligi hiyo Manchester United kwa bao moja kwa bila katika uwanja wa Anfield.
Hii ni mara ya kwanza kabisa kwa Liverpool kuwa katika nasafi kama hii mwanzo mwanzo wa ligi tangu mwaka 1995.
Pia Liverpool inakuwa timu ya kwanza tangu mwaka 2011 kucheza mechi tatu mfululizo katika ligi hiyo bila ya kufungwa goli lolote.
Ilikuwa fursa nzuri kwa kuhitimisha miaka 24 tangu kuzaliwa kwa kuipatia Liverpool bao hilo la pekee na la ushindi.
Mwamba huyo alifunga bao hilo kwa ustadi mkubwa kwani alifunga kwa kichwa safi ambapo kipa wa Man U De Gea alishtukia wavu ukitikisika.
Ni mara ya tatu mfululizo kwa Sturridge kuivungia timu yake tangu ligi hii ya Uingereza ianze.
Daniel Sturridge mfunganji wa Liverpool
Kushindwa kwa Manchester United inachafua rekodi ya kocha wao mpya David Moyes kwani hata akiwa mkufunzi wa Everton hajawahi kuingozi timu yake kuifunga Liverpool katika uwanja wa Anfield.
Hata Robin van Persie alikuwa na siku mbaya kwani alikuwa na wakati mgumu kumfunga kipa mpya wa Liverpool Simon Mignolet, ambaye alizima ndoto ya Man U ya kupata bao.
Tangu mlinda lango huyo Mignolet, kuhamia Anfield kutoka Sunderland kwa kima cha £9m hajafungwa bao hata moja.

Orodha ya wachezaji

Liverpool
22 Mignolet
02 Johnson (Wisdom - 79' )
03 Jose Enrique
05 Agger
37 Skrtel
08 Gerrard
09 Aspas Booked (Sterling - 60' )
10 Coutinho (Alberto - 84' )
14 Henderson
21 Lucas Booked
15 Sturridge
Wachezaji wa akiba
01 Jones
34 Kelly
38 Flanagan
47 Wisdom
06 Alberto
31 Sterling
33 Ibe
Manchester United
01 De Gea
03 Evra
04 Jones (Valencia - 37' )
05 Ferdinand
15 Vidic
11 Giggs (Hernandez - 73' )
16 Carrick Booked
18 Young Booked (Nani - 63' )
19 Welbeck
23 Cleverley Booked
20 Van Persie Booked
Wachezaji wa akiba
13 Lindegaard
12 Smalling
28 Buttner
08 Anderson
17 Nani
25 Valencia
14 Hernandez

Arsenal waifunga watani wao wa jadi wa london Tottenham kwa goli moja kwa bila



 2Septemba, 2013 
o ya kutofungwa na Tottenham katika uwanja wao wa nyumbani baada ya kuwazaba vijana wa Andre Villas-Boas bao moja kwa sufuri.
Arsenal waifunga Tottenham
Tangu mwaka wa 1993 Tottenham imewahi kuifunga Arsenal nyumbani mara moja tu.
Kwa kocha huyo mreno ni siku ya masikitiko kwani ndio mechi yake ya kwanza kwa timu yake kupoteza tangu msimu huu uanze.
Ilikuwa ni katika dakika ya 23 wakati Olivier Giroud alipofunga baada ya kupewa pasi na Theo Walcott .
Katika dakika za lala salama za kipindi cha pili licha ya Tottenham kujenga hema katika ngome ya Arsenal lakini kipa Wojciech Szczesny alifanya kazi ya ziada kwa kuokoa mkwaju wa Jermain Defoe hivyo kuwanyima vijana wa Villas-Boas nafasi ya kulikomboa bao hilo.
Ushindi huu unamaanzisha kuwa vijana wa Arsene Wenger wamepanda hadi nafasi ya nne katika jedwali la ligi hiyo ya Uingereza.

Orodha ya Wachezaji

Arsenal
01 Szczesny
04 Mertesacker
06 Koscielny
25 Jenkinson
28 Gibbs
07 Rosicky Booked (Monreal - 79' )
10 Wilshere (Flamini - 43' Booked )
14 Walcott (Sagna - 90' )
16 Ramsey
19 Cazorla
12 Giroud
Wachezaji wa akiba
21 Fabianski
03 Sagna
17 Monreal
20 Flamini
44 Gnabry
58 Gedion Zelalem
22 Sanogo
Tottenham Hotspur
25 Lloris
02 Walker
03 Rose
05 Vertonghen
20 Dawson
08 Paulinho
15 Capoue (Sandro - 75' )
17 Townsend (Lamela - 75' )
19 Dembele (Defoe - 69' Booked )
21 Chadli
09 Soldado Booked
Wachezaji wa akiba
24 Friedel
16 Naughton
14 Holtby
22 Sigurdsson
30 Sandro
33 Lamela
18 Defo

Bale avunja rekodi ya dunia ya uhamisho

 2 Septemba, 2013 
Gareth Bale
Gareth Bale
Real Madrid imevunja rekodi ya dunia ya uhamisho wa wachezaji kwa kumsajili mshambuliaji wa Tottenham Gareth Bale.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Wales ametia saini mkataba wa kuichezea Real Madrid wa miaka 6 kwa kununuliwa kitita cha pouni milioni 85,3.
Rekodi iliyokuwepo ilikuwa ya Cristiano Ronaldo aliponunuliwa na Real Madrid toka Manchester United kwa pouni milioni 80 mwaka 2009.
"nilikuwa na furaha ya miaka 6 niliyochezea Spurs,lakini huu ni wakati mwafaka kwangu kusema kwa heri "alisema Bale mwenye umri wa miaka 24.
Bale aliyeshinda tuzo ya mchezaji bora wa msimu uliopita katika ligi kuu ya England alijiunga na Tottenham kutoka Southampton kwa pouni milioni 10 mwaka 2007 na alifunga magoli 26 msimu uliopita.