Sunday, August 31, 2014

Hodgson:England haijapoteza uelekeo


Kocha wa England Roy Hodgson
Kocha wa timu ya Taifa ya England Roy Hodgson amesema England haijapoteza uelekeo wakati ikijiandaa na michuano ya kombe la ulaya mwaka 2016, na kuelekea kampeni za kufuzu kushiriki michuano hiyo, kampeni zitakazoanza mwezi ujao.
England ambayo ilishindwa kufanya vizuri kwenye michuano ya kombe la dunia katika hatua ya makundi itaanzia kampeni yake ugenini kwa kupambana na Switzerland tarehe 8 mwezi Septemba.
Katika katika kundi iliyopangwa, England itapambana na timu za Slovenia,Estonia, Lithuania na San Marino.
Hodgson amesema ana matumaini kuwa watafanya vizuri.
England imeshuka kiwango cha ubora vya fifa mpaka nafasi ya 20th baada ya kuchemka nchini Brazil walipopoteza mchezo dhidi ya Italia na Uruguay, kabla ya kupata pointi dhidi ya Costarica ambapo tayari walikuwa wametolewa.

No comments:

Post a Comment